Sura ya Tano

22 2 0
                                    

Siku ya upasuaji wa Suzzanna kama ilivyoratibiwa na daktari  Mathangi iliwadia.
Mathangi alihakikisha kila alichokihitaji kufanya upusuaji kilikuwa tayari.
Kitanda cha kumlaza mgonjwa kilikuwa kimetandikwa na hata kupuliziwa manukato yaliyoacha mapua wazi kwa mvutio.
Koja la maua lilijipanda pembeni,likiashiria ni chumba chenye uhai na starehe.
Godoro aina ya 'Dreamland' lilikilalia kitanda na kukifanya kunyooka twa! tayari kumkandakanda  mgonjwa na kumwacha katika usingizi wa pono.
Shuka za rangi nyekundu zilikivaa kitanda na kukifanya  kuonekana kama tandiko la malkia kwenye kasri.
Mziki aina ya 'blues' uliyoimba na sauti za kumvutia nyoka kutoka pangoni,uliporomoka kutoka kwa radio aina ya 'Sonnymax'.
Mvinyo aina ya 'red wine' ulikuwa umeandaliwa kwa unadhifu,ukiambata na glasi mbili tayari kumutumbuiza mgonjwa na kumuliwaza ili kumfanya kupitia upasuaji bila haya.
Mataa yaliyomulika kwa mwanga mwekudu na samawaki yalimetameta kwa zamu na kukipaka chumba cha upasuaji kubadilibadili rangi kama kinyonga.
Kila kitu chumbani kikichukua rangi za mataa kisitambulike rangi yake halisi.
Kinyume na mazoea katika upasuaji wa hapo mbeleni;wakati huu Mathangi hakukusudia kuvalia glavi katika mikono yake.
Angefanya upusuaji mikono uchi.
Pengine alimwamini mgonjwa huyu zaidi,kuamini hangemwambukiza maradhi yeyote.

"Kokoko"  mlango ulibishwa kwa mpigo dhaifu.
Mgonjwa alikuwa keshawasili.
Mathangi alikipiga macho chumba chote kuakikisha kila kitu kilikuwa sawia,kwa mara ya mwisho,kisha akaelekea mlangoni kumkaribisha mgonjwa.
Kulikuwako na kamera ya siri mlangoni iliyomwezesha kutimazama aliyekikaribia chumba hiki akiwa mbali.
"Karibu,Karibu ndani Suzzie" alimpiga pambaja haraka haraka huku akimunyooshea mkono kumkaribisha ndani.
Alichunguliachungulia nje kwa mpepesuko, kuhakikisha kuwa hakukuwa na mtu mwingine karibu, kabla ya kuufunga mlango kwa funguo.
"Wao this place looks so romantic" mgonjwa alitamka huku akizungukazunguka chumbani,akichezachezesha kiuno kuandamana  mdundo wa mziki uliokuwa ukiporomoshwa kwa sauti nyororo ya Lionel Richie.
"Karibu kwa kitanda" Mathangi alimkaribisha huku akimkabidhi glasi iliyojazwa mvinyo.
"Ahsante!" mgonjwa aliketi pembeni mwa kitanda na kuuweka mguu mmoja juu ya mwingine na kuyawacha mapaja yake meupe pepe!wazi.
Msisimko ulimpanda Mathangi na kumwongezea matumaini ya kukamilisha upasuaji huo.
"You look so lovely!" Mathangi alitamka huku akiupitisha mkono wake juu ya mapaja ya mgonjwa.
Mgonjwa hakumzuia bali alimwacha kujibamba.
Mgonjwa alipiga funda kubwa la mvinyo huku akisimama na kumkalia daktari mapajani.
Unyororo na joto la makalio lilimwacha daktari akidodokwa na mate.
Ili lilimpata Mathangi kwa mshangao.
Mambo yalikuwa yanaenda upesi kuliko alivyotarajia.
Akiupitisha mikono wake katika kiuno cha mgonjwa na kuyakamata maziwa yake huku akiyafinyafinya kwa utaratibu.
Mgonjwa aliachilia sauti ya kuridhika na kupumua huku akifunga macho.
Uhodari wa mokono ya daktari ulimfanya kuisahau ghadhabu yake kwa muda.
Mikono ya daktari ilipofikia nywele zake za kifarasi, mgonjwa alisimama haraka kujinasua.
Palikuwepo kamera ya kisiri katika nywele zake iliyotumiwa na majasusi kufuatilia sinema hii.
"Naomba twende kwa upasuaji moja kwa moja kwa sababu nina shughuli zingine" mgonjwa aliomba huku akimrusha daktari kifudifudi kitandani.
Alilifungua shati la daktari huku akimpapasapapasa kwa vidole vyake vyororo.
Kwa zamu walivuana nguo na kubaki uchi wa nyani tayari kuuanza upasuaji.

"Taptap!taptap!" sauti za watu wakikaribia kwa utaratibu zilisikika.
Mathangi alimrusha Suzzie pembeni na kukimbilia mlangoni kuchungulia akitumia kamera ya siri.
Aliwaona wanaume watatu na wanawake wawili waliojihami kwa bastola wakikaribia mlango.
Nyuma yao wanahabari walifuata unyounyo tayari kunasa uvamizi huo.

Suzzie aliangukia meza na kuumia vibaya.
Kamera iliyobandikwa nyweleni ilivunjika na kutapakaa vipande vipande,juu ya michirizi ya damu iliyomtoka Suzzie kichwani.
"Pu!" makachero waliupiga mlango dafrau na kujitosa ndani wazimawazima tayari kumkamata Mathangi.
Mathangi hakuwepo.
Walitaftatafta chumba kizima wasimpate.
Suzzie alikimbizwa hospitalini akiwa amepoteza fahamu.
Baada ya uchunguzi wa kina majasusi waligundua mpenyo wa chinichini kule chumbani,alioutumia mshukiwa kukwepea.
Mathangi alikuwa amewaponyoka.

SUZANNAWhere stories live. Discover now